Mkuu wa mkoa wa Mara, Ally Hapi amewaapisha wakuu wa wilaya za mkoa wa Mara ambapo miongoni mwa waliopishwa ni pamoja na Juma Chikoka maarufu kama Mchopanga kuwa mkuuwa wilaya ya Rorya, Joshua Nasari kuwa mkuu wa wilaya ya Bunda na Dk Vicent Mashinji kuwa mkuu wa wilaya ya Serengeti ambapo wakuu hao wa wilaya kwa nyakati tofauti wameomba ushirikiano kutoka kwa wakazi wa mkoa wa Mara na viongozi wote.